UFUGAJI: njia za ufugaji wa ngombe wa kisasa na jinsi ya kupata faida yake

Tanzania ni moja ya nchi zenye mifugo mingi Africa, hasa ng'ombe wa kienyeji, lakini uwingi huu unaonyesha hauonekani na hauendani sambamba na kipato cha mfugaji. Jambo hili limegubikwa na changamoto nyingi sana. Hili tutaliongelea siku nyingine.
Image result for jinsi ya kufuga ng'ombe wa maziwa
Leo hebu tujikite katika ufugaji wa ng'ombe wa Maziwa na Aina zake. Tunapoongelea ng'ombe wa Maziwa tunajielekeza katika makabila ya ng'ombe wa Maziwa wa kigeni. Makabila haya yaliingizwa na kuendelezwa hapa nchini kitaalamu hasa miaka ya 1974 pale Mwalimu Nyerere alipoona uhitaji wake na kwenda kuwaomba wamarekani wamsaidie, Shirika la Kimataifa la Mitamba, HEIFER INTERNATIONAL, ndio waliopewa jukumu hilo la kusimamia mradi huo mkubwa na ilibidi watafutiwe sehemu yenye hali ya hewa inayoendana na walikotoka. Waliwekwa katika shamba la Kitulo na kuzalishwa na kuendelezwa pale kitaalamu.
Ng'ombe hawa hula chakula kingi na kunywa maji mengi tofauti na wale wetu tuliowazoea wa kienyeji. Pia ng'ombe hawa si wavumilivu sana kwa magonjwa, Kwa hiyo mfugaji lazima uwe karibu sana na mfugo wako.
Katika kuhakikisha kwamba ng'ombe hawa hawapati maambukizi ya magonjwa na wanaweza kupata chakula cha kutosha, inashauriwa wafugiwe ndani na kuhudumiwa kila kitu ndani.
Ng'ombe hawa wakifugwa vizuri na kuhudumiwa vizuri wanaweza wakatoa kuanzia Lita 10 hadi Lita 50 kulingana na kabila la ng'ombe. Kwa hiyo wakulima na wafugaji wadogo wadogo wanaweza kupata maendeleo ya haraka na yenye tija Kwa kufuga ng'ombe wa aina hii.
Katika mjadala wetu huu tutaangalia pia jinsi ya kuwaboresha ng'ombe wa kienyeji ili kuongeza tija katika utoaji wa Maziwa.
AINA ZA NG'OMBE WA MAZIWA.
Zipo aina tatu kuu za ng'ombe wa Maziwa ambazo ni;
i. Halisi (pure)
ii. Chotara (cross)
iii. Asilia
Ng'ombe halisi: Ng'ombe huyu ni yule asiye kuwa na mchanganyiko wa damu ya kabila jingine.
Makabila ya Ng'ombe Halisi.
Yapo makabila mengi ya ng'ombe wa Maziwa. Lakini kwa Afrika mashariki yapo makabila maarufu matano;
i. Friesian
ii. Ayrshire
iii. Jersey
iv. Guernsey
v.  Brown Swiss
Hayo ndio makabila ya ng'ombe wa Maziwa. Katika makala inayofuata tutaanza kuchambua kabila moja baada ya jingine ili kuweza kujua sasa jinsi ya uzalishaji wake wa Maziwa na ulishaji.

Comments

Popular posts from this blog

Jifunze kuhusu mbilimbili na matumizi yake yote

MAAJABU KUHUSU MAFUTA YA MAWESE

JUA KUHUSU UGONJWA WA BAWASIRI